Sehemu ya 1
1. Mungu Aliumba Dunia Kamilifu
Mungu ndiye Muumbaji, mwasisi na mbunifu wa kila kitu kuanzia nyota zinazotoa mlipuko wa mwanga mkubwa kuliko jua na kutoweka (supernovas) hadi mabawa ya kipepeo.
Zaburi 33:6-9
“Kwa neno la BWANA mbingu zilifanyika na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake.... maana yeye alisema, ikawa; na yeye aliamuru, ikasimama.”
Mungu hana budi kusema tu, kisha vitu vya asili hutii mapenzi yake.
